Friday, September 2, 2011

Dadi na Mami


Dadi achana na mami

Vita ni vya nini

Hakuna amani

Mami pendana na dadi

Amekosea sawa

Hakuna msamaha



Sikujui sikutambui

Wewe ni nani, Jitambulishe

Mpenzi wa mami, baba yangu

Hatupigi, si desturi yake

Maneno hayo, uyasemayo

Hayafai na mchungaji

Tupe muda tujipumzishe

Mafichoni chini ya kitanda



Twatafuta upendo usiopo

Pahali pa busu, nusura kifo

Majirani hamtusikii

Kumejaa dhiki, baba mnafiki

Tumbo njaa, ngumi shibe

Askari okoa, njooni mumshike

Haya tosha, hatutaki tena

Kila mmoja paa, tujikimbize





Sitaki kusema kwaheri

Sitaki kukubali imeisha kati yetu

Sitaki kusema, sitaki kukuona

Nataka kusema, see you kesho

Sitaki ku-let go

Siko tayari kuku-lose natamani kuwa karibu nawe, nawe….

No comments:

Post a Comment